16/12/2011

SOMA CHUO CHA HAVARD BURE

Usishutuke na wala sio utani. Tunaweza kweneda havard  na kusikiliza lekcha bila wewe kupanda ndege. Gharama utayotumia ni  ndogo sana. Ukisikia dunia imekuwa kama kijiji ni sababu na  faida na Fursa zinazoletwa na TEKNOHAMA

15/12/2011

NDANI YA KIWEKA DATA(HDD) KUNANI

Siku chache zilizopoita katika forum maarufu ya ya jamii forum kuna mjumbe aliwasilisha tatzo la HDD yake. Tatizo lile lililifanya na lilinipa nguvu ya kufanya kitu ambacho nilipanga kukifanya sikuuuuu nyingi lakini sikuwa na mwammko au muda. Ni kitu gani hicho??? Ni kuangalia kuna vitu gani ndani ya Hard  Disk  Drive (HDD)
Katika makororo yangu ya kompyuta nilikuwa nina HDD ya Maxtor ya 20GB amabayo ilikwua mbovu. Zaidi ya HDD kilichohitajika  kingine ni screw driver sahihi.
Yafuatayo ni maelezo ya picha nilizopiga mwenyewe na ufafanuzi wa sehemu mbali mbali za HDD. Kumradhi kwa quality duni ya picha lakini ni matumanini yangu ujumbe uliokusudiwa utaelewekwa bila tatizo
Kwanza tunaaza kufungua screw zinazoshiikilia kasha
Mara nyingi HDD zina rangi ya shaba. Juu ya HDD kuna maelezo mbali mbali mbali kama y size, Pembeni kuna Seheumu za HDD kupokea moto kutoka kwneye Poer supply. Pia kuna waya (Data bus) ya kupokea datakutka na wenda kwenye motherboard.  HDD Inaweza kuwa ni ya IDE au SATA.
Srew nyingine zimefichwa
Katila kuhakikisha kuwa wanagundua  mtu akikiuka masharti ya wararty kuna srew nyingine zinafichwa chini ya label . Kufungua azima uchane label. Ukichana label then warannty hakuna . Hii ni HDD mbovu tunaendelea. Katika picha hii kwenye HDD unaweza uona kuna malezo mengi juu ya HDD husika.Kuna maelezoni jinsi gani HDD inaweza kufanywa kuwa master au Slave.

HDD circuit board aka motherbard ya HDD
Circuit board hii ndio ubongo wa HDD inayoongoza utendaji kazi wa vifaa mbai mbali ndani ya HDD.  Nimeipachika jina la motherboard ya HDD .Hapa ukifungua screws zilizoshikilia ubao huu basi unaweza utenganishwa na kasha la Hard Disk
Mawasiliano ya Circuit board na HDD
Kilichoishangaza hakuna waya waya  zinazounganisha HDD na  circuit board. Mawasiliano  yanafanyika kutumia vitu kama spring.Waliobobea wenye mamb ya electoniki wanaweza kujua sababu ya hili. Tunaweza kuuuliza pia kwa nini circut board zinakuwa na rangi ya kijani?

Platters and Read/Wrte heads
  Ganda la HDD likiondolewa  tunaona kitu kama kisahani(platter) Hii ndio disk yenyewe. Pia kuna  kichwa chakusoma na kundika data kwenye kisahani. Kwa jina la kitaalam kinaitwa Read/Wite heads. Kisahanikinangara   sana na  inashauriwa  kazi hii ifanyike kwenye chumba kisafi sana. Kama nilivyosema sijali sana sababu hii ngoma ilishaharibika siku nyingi

Mkono wa kuandika na Kusoma

Na hapa  ndio electroniki za “mkono” unaotmika kuanidka na kusoma data kutoka na kwenda kwenye kisahani zilipo. kumbuka utendaji kazi wa haya yote unaogozwa na na circuit board.
Kwa leo tuishie hapo . Tutavipingua zaidi vifaa vingine siku nyingine. Kama una chochte cha kuongeza kupunguza kuponda  usisiste kuacha maoni

17/11/2011

Sifa za mwanateknik bora

Moja kwa moja kwenda hoja .Haya ni baadhi ya mambo yanayoweza kufanya mtu yeyote kuwa katika nafasi ya kujiita mwanateknolojia bora mwenye taarifa sahihi na za wakati.natarji wazefu  wataongeza zaidi

1. Jifunze jambo au habari mpya kila siku.

Kwa kutumia gooogle na mitandao mbali mbali mbali ni rahisi kujifunza mambo mapya ya kitenolojia. Changamoto ni chanzo ni chanzo na habari gani hasa zina mafunzo. Kutokana na uelewa , fani tofauti watu tuna prority tofauti
Mfano zaidi ya jf tovuti nyingine ambazo binafsi natumia kujifunza na kupata tech news ya issue mbali mbali ni Dailytech, Techcrunch, Click Online
Cha msingi watu tuelewe internet ina kila aina ya habari nzuri na ina kila aina ya habari za ajabu. Mfano nimeona hapa kuna baadhi ya member wanapost article za kuhusu virus amabazo sio za kweli.(Hoax) Ujumbe unaasema eti virus ataburn the whole HDD. Hivi kuna virus anaweza kuunguza HDD.??????. So tusiamini na kucukua kizima kizima kila tunachoona kwenye net. Some time tuchunguze na tujirizishe.

2. Fanyia kazi na jaribu mambo kwa vitendo

Binafsi naona watanzania wengi tumeridhika na utaalam wa theory. Ikija kwenye nadharia na vitendo tunakwama na kukutana na vikwazo vingi. Hii inatokana na watu kuridhika nadhiria kitu amabcho si kizuri sana. Kifupi hatupendi kupigika. Ninafanya kazi na mtu ambaye hapendi kuonekana kashika cripping tool. Alanachukia kweli kuitwa fundi au techinician Teh teh teh. Yeye anataka aitwe Network admin au engineer.
Mwisho wa siku tunakuwa na vyeti safi lakini hatuna good practical experince………….


3. Jiulize na uliza maswali magumu

Kuna wataalamu hawapendi au wanaona aibu kuonekana wanauliza maswali .Binafsi naamin tutakuwa watalmu bora kama tutakubali kuwa una wakati tunaweza kuwa “wanafunzi” na kuna wakati tunaweza kuwa “walimu”. Pausing kama mwalimu tuuuu au kama mwanafunziii tuuuuuuu siku zote haiwezi kumjenga mwanateknolojia. Na hata wanasiasa..
Jiulize zaii di na zaidi
maswali magumu
Chimba zaidi uelewe zaidi
Mfano una watu nimeona wanajiuliza maswali ya kuchakachua TV decoder ili wapate channel za bure. Lakini sio wengi wa watu hawa wamejiuliza swali gumu kwanza la HowStuffWorks “Satellite TV System”.. Mtu akisoma articles mbali mbali kuhusu hili anaweza kujua urahisi na ugumu wa kuchakachua channel na atauwa kajifunza.

Tofauti ya DVD na CD ni Nini? Haraka haraka jibu ni kwamba DV ina size kubwa. Lakini tuendelee tjaribu kujiliza swali gumu. Kwa nini DVD ina uwezo mubwa wa space na C ina uwezo mogo waati kimaumbile zote ni sawa? . Kwa hiyo tujaribu kchimba na kuelewa kiundani. La sivyo tutajikuta tunajiita wataaam tunatoa maelezo amabayo sio ya kitaalam.
Mtu akikuuliza kama mtaalam unajirate vipi utaalam wako wa iwe ni ICT, umeme programming, etc .? Wewe ni Advanced, Avarage or just end user. Binafsi i treat myself an avarage but competent ICT techician.

4. Penda majadiliano endelevu

kuna baadhi ya watuu hapa kwenye teknoloja na hata huko kwenye siasa na majukwaa mengine hawapendi kutoafautiana kwa mawazo, approach na ideas.. ..Ukimkosoa kitu anakuona adui au anakuwa mkali Vile vile kuna wale wengine kwa kuwa wajua sana akiona mtu anafanya au kaandika kitu fulani anamponda. Tena mbaya zaidi kwa lugha ya dhiaki.

Majadiliano
Mijada ni muhimu katika kukuza ujuzi
Tunachotakiwa kufanya ni simple kwanza tukubali kutaofautina na pili tukubali na tukaribishe majadiliano endelevu kwa lugha nzuri..



5. Wezesha end user kutatua matatizo yao wenyewe

Kuna watalaam wanapenda kuendelea kutatua matatizo madogomadogo badala ya uwaambia wahusika nini cha kufanya wenyewe. huu unaweza kuwa ni uchoyo na vile vile kuna watu hawapendi kufuata proceure kusoma manual ya vifaa vyao huu nao ni Uvivu mbaya. So upande wa wataalam ni vizuri kuwawezesha watu kutatua matatizo madogo madogo ili wasisumbe tena na upande wa watuamiji wa kawiada uipta tatizo soma manual yakifaa au tafuta manua ya kifaa mtandaoni.
Tegua kitedawili: Je dereva asiyependa kuchafuka lakini anaelewa vema kueleazea kila kifaa cha gari yake ni mwanateknolojia bora Kuliko fundi anayealitenegza gari hilo kila likiharibika?
Je kuna jambo nimeliacha, nimekosea au sijaligusia?usisite kunikosoa kuongeza au hata kuchakachua…..